Ni usemi wake mshauri wa serikali hiyo ya kaunti kwa maswala ya uongozi ali Musa Chibole

Kwenye mahojiano ya kipekee na idhaa hii Chibole amesema kuwa serikali ya kaunti ya Kakamega huwalipia karo watoto werevu kutoka jamii zisizo jiweza kama njia mojawapo ya kufanikisha masomo yao

Chibole hata hivyo amelaumu uhamisho wa walimu hadi sehemu tofauti kama baadhi ya visababishi vya kudorora kwa viwango vya masomo kwenye kaunti hiyo

Kuhusu hali ya uhaba wa dawa kwenye baadhi ya hospitali eneo la magharibi Chibole amewasuta baadhi ya wafanyikazi kwenye idara ya afya tatizo hilo akiapa kuchukua hatua zifaazo 

Haya yanajiri huku tatizo la uhaba wa dawa likizidi kushuhudiwa kwenye vituo kadhaa vya kiafya kikiwemo cha shianda na kile cha makunga eneobunge la Mumias Mashariki

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE