Serikali ya kitaifa inazidi kulaumiwa kwa kukosa kutekeleza sheria ambazo ziliwekwa za kudhibiti matumizi ya bidhaa za Tumbaku humu nchini jambo linalochangia kampuni zinazotengeza bidhaa hizo kuendelea kufaidika huku afya ya wananchi ikiwa hatarini
Haya ni kwa mujibu wa mwenyekiti wa muungano wa kudhibiti matumizi ya Tumbaku nchini KETCA Joel Gitali akizungumza mjini Kakamega, ambaye ameisuta serikali kwa kukosa kuhakisha sheria zilizowekwa kudhibiti matumizi ya tumbaku nchini zinafwatwa kikamilifu bila ya kuzingatia madhara yake kwa wananchi
Gitali amesema kuwa kampuni zinazotengeneza na kuuza bidhaa hizo humu nchini zimenufaika pakubwa licha ya kuwepo kwa mikakati na mashirika ya kudhibiti kampuni hizo huku akiitaka serikali kuajibika na kuingilia kati
By Lindah Adhiambo