Serikali ya kaunti ya Kakamega imeanzisha mchakato wa kuwahamasisha  wakulima wa kaunti hiyo kuhusu kilimo cha samaki na nia ya kukiimarisha kilimo hicho ili kuinua kiwango cha uchumi miongoni mwao.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo katika boma la mkulima mmoja maeneo ya Shisiru wadi ya Butsotso ya kati eneo bunge la Lurambi, afisa inayesinamia idara ya ufukaji wa Samaki kaunti ndogo ya Lurambi Japheth Juma amesema kuwa serikali  ya kaunti hiyo imejitolea kuwawezesha wakulima hao  kwa kuwapa mahitaji yanayofaa kilimo hicho.

Wakati huo uo afisa huyo amedokeza kuwa eneo hilo liko na uwezo wa kukuza Samaki kwa wingi huku akiwataka wakulima kukumbatia mradi huo ambao serikali inapeana ufadhili wa asilimia 50 kupiga jeki kilimo hicho .

Kwa upande mwingine wakulima waliohudhuria mafunzo hayo walipongeza  serikali kwa kuanzisha mradi huo  wa samaki  na kutaka wengine ambao bado  hawajajiunga kufanya hivyo ili waweze kung’atuka katika lindi la ufukara .

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE