Wafanyi  biashara  wa  soko  la  Kambi-Mwanza  lililo  katika  kaunti  ndogo  ya  Malava  kaunti  ya  Kakamega,  wanalilia  hali  ya  soko  hilo  kuwa  hairidhishi  kwa  upande  wa  usafi.

Wakiongea  kupitia  kwa  mwenyekiti  wao  kina  mama  wanaouza  samaki  kwenye  soko  hilo,  Hellen  Luseno  anaelezea  jinsi  wanavyopitia  changamoto  zikiwemo  usalama  wa  sehemu  ya  kuuzia  samaki  kwamba  vibanda  vyao  huvunjwa  na  kuwafanya  kukosa  amani.

“Soko ya kambi wameeka nyumba mingi na vibanda vinavunjwa mara kwa mara. Hatuna ata choo na soko la chakula linafaa kuwa safi” alisema mwenyekiti

Mwenyekiti  huyo  anaiomba  serikali  ya  kaunti  ya  Kakamega  kupitia  kwa  gavana  Wycliffe  Oparanya,  kuangalia  hali  ya  soko  hilo.

Anasema  kwamba  ombi  lao  ni  kuhusiana  na  msimu  ujao  wa  mvua  ambao  utawatatiza  mno  kwani  mahala   pa  kujikinga  wakiendesha shughuli  zao  za   biashara  ni  kizungu-mkuti.


“ Naomba serikali ya kaunti kujenga mahali pa kujikinga mvua katika soko ya kambi na pia watujengee vyumba vya kujisaidia.”

Story by Sajida Wycliff

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE