Wenyeji wa Kaunti ya Trans-Nzoia wanatarajiwa kufaidi msaada wa   neti  600,070 ya kuzuia msambao wa mbu inayosababisha maradhi ya Malaria nchini. 

Akihutubu kwenye mkutano wa hamasisho kwa washikadu katika sekta ya afya, waziri wa afya Kaunti  ya Trans-Nzoia Bi Clare Wanayama amesema kaunti ya Trans-Nzoia inashuhudia  3% ya msambao wa malaria dhidi ya  8%  kote nchini, akisema wizara yake inalenga kutoa matibabu kwa  watakao ambukizwa  malaria  bila ya kupoteza maisha ya yeyote Kaunti hiyo.

Kwa  Upande wake Dkt Philip Bett mkurugenzi wa maswala ya kukabili maambukizi ya malaria Kaunti ya Trans-Nzoia ameelezea umuhimu wa matumizi ya Neti ya kuzuia mbu na msambao wa ugonjwa wa  malaria, akiongeza kuwa Neti hizo zitatumika kwa zaidi ya miaka mitatu. 

By Imelda Lihavi

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE