Chama cha UDA  kinacho husishwa naye Naibu Rais dakta William Ruto kimezindua zoezi la kuwasajili wanachama katika eneo bunge la Likuyani katika juhudi za kukipa umaarufu na uungwaji mkono  mashinani mbele ya uchaguzi mkuu mwaka ujao.

Akizungumza alipozindua  zoezi hilo kwenye hafla iliyooandaliwa  katika eneo la Soy, kaimu mwenyekiti wa chama hicho tawi la Likuyani Deberious Shikuku Wafula amefichua kuwa tayari chama hicho kimewa vutia zaidi ya wafuasi elfu 15 eneo hilo , akihoji kuweka  mikakati ya kuuza sera za chama hicho mashinani na kuhakikisha kinashinda viti vingi mno kwenye uchaguzi mkuu ujao. 

Aidha Deberious amepuuziliambali madai kuwa eneo la magharibi ni ngome ya vyama vya ANC na Ford Kenya.

By Richard Milimu

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE