Akiongea kwenye mazishi ya mama Dina Achimbo eneo la Elukho Butsotso Mashariki askofu Naftali Malanga wa kanisa la Church of God Ingotse mission kanda ya kati amesema kama kanisa wako tayari kuendeleza masharti ya kuthibiti msambao wa corona
Naibu chifu wa kata ndogo ya Indangalasia Scholastica Jirongo ambaye alihudhuria mazishi hayo amewahimiza wananchi kuzingatia mwongozo ambao umepeanwa na wizara ya afya
Bi Scholastica vile vile amewahimiza wazazi kuona kwamba wanapeleka watoto shuleni juma lijalo
Wazazi watoto wenu waende shule wakati shule zinafunguliwa. wasibaki nyumbani kwamaana sitaruhusu kabisa nitatembea nyumba kwa nyumba kuhakikisha watoto wote wa umri ya kwenda shuleni wanameenda shuleni.
By Lindah Adhiambo