Vuguvugu la Youths for Mulasia linalounga azma ya Kiongozi wa ANC ya kuwania urais mwakani sasa linamshinikiza naiburais kujiuzulu iwapo haridhiki na uongozi wa serkali iliyopo

Katibu wa vuguvugu hilo Kanda ya Magharibi Brian Amakobe amemtaka Ruto kuondoka serikalini badala ya kuilaumu kila uchao

Amakobe amesema kuwa serikali ya jubilee imefeli kuwahudumia Wakenya na Ruto ni sehemu ya uongozi huo

Kiongozi huyo amemsuta mbunge wa Mumias Mashariki Ben Washiali kwa kuchangia kudorora kwa uchumi eneo hilo

Kiongozi huyo amechukua fursa hiyo kumpigia debe Kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi akisisitiza kuwa ndiye aliye na uwezo wa kuufufua uchumi wa taifa hili unaozidi kudorora

By Richard Milimu

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE