Chifu wa Butsotso Mashariki kaunti ya Kakamega Justus Mukoshi amewataka vijana wanaotoka mashinani kutafuta ajira mijini kuwaelezea wazazi kuhusu maeneo yao ya kazi kuepuka sintofahamu

Akiwahutubia waombolezaji katika kijiji cha Emusala kwenye mazishi ya kijana Abraham Nambala ambaye alifariki katika hali tatatanishi baada ya kuondoka nyumbani mwezi Februari, Mukoshi amesema ni muhimu kwa wanafamilia kujua waliko wapendwa wao


Aidha chifu Mukoshi amewataka wakazi kuzingatia masharti ya kuthibiti corona na kujitokeza kwa chanjo wakati serikali itakapo tangaza bila kupotoshwa kuhusu madhara ya chanjo

Kwa upande wake naibu wa chifu wa kata ndogo hiyo ya Indangalasia Scholastica Jirongo amekashifu ongezeko la dhuluma za kijinsia


By Lindah Adhiambo

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE