Wakaazi wa lokesheni ndogo ya Buyangu wamehimizwa kuzingatia sheria za kudhibiti msambao wa virusi vya corona 

Ni kauli yake naibu chifu wa lokesheni hiyo Catherine Nelima akihutubia waombolezaji kwenye ibaada ya maombi na mazishi ya mzee Renson Oyangi Magana katika kijiji cha Lusero 

Nelima amewahimiza wazazi kuwapeleka wanao waliokalia mtihani wa kitaifa wa darasa la nane KCPE mwaka uliopita ikizingatiwa agizo la serikali la kuhitimu asilimia 100

Naye mwakilishi wadi wa Isukha Kazkazini eneo bunge la Shinyalu kaunti ya Kakamega Hellemina Llanziva akiwahutubia waombolezaji amewatahadharisha wakaazi wake dhidi ya tapeli wanaokusanya kadi za kitaifa na kuwasajili wakenya katika mirengo mbalimbali ya kisiasa kwa kutojua huku uchaguzi mkuu ukikaribia

Llanziva amewataka viongozi na wanainchi kutimiza amani taifa linapokaribia kwenye uchaguzi mkuu akiwataka wakaazi kuwa makini na waangalifu wakati wa uchaguzi mkuu 

By Sajida Javan

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE