Wakaazi wa mkoa wa magharibi mwa Kenya wametakiwa kumuunga mkono kinara wa chama cha ANC Wycliffe Musalia Mudavadi kwenye uchaguzi mkuu ujao 

Ni kauli yake mbunge wa Malava Moses Malulu Injendi akizungumza kwenye mahojiano na kituo cha 102.2 Lubao fm

Malulu amesema Mudavadi anao uwezo wa kulikomboa taifa hili haswa katika swala la kiuchumi akimlinganisha na rais wa tatu wa jamhuri wa Kenya

Malulu pia akiipuzilia mbali misimamo kinzani ambayo amekuwa nayo hapo awali akisema imepitwa na wakati na kwa sasa ni wakati wa kutembea naye Mudavadi 

Malulu amewataka viongozi wa Magharibi kuja pamoja na kumuunga mkono Mudavadi na kuondoa tofauti zao za kisiasa ili kujipa nguvu kwenye serikali itakayobuniwa baada ya uchaguzi mkuu ujao 

Malulu ametabiri uwezekano wa viongozi tokea Mlima Kenya ambao amesema ikikaribia kwenye uchaguzi mkuu ujao watamuacha Naibu wa Rais William Ruto

Wakati uo huo Malulu ameunga swala la kuwataka viongozi wawe na shahada kwenye uchaguzi mkuu ujao kwa wabunge na kurekebishwa kwa kipengee cha wakilishi wadi na wale wa kike kwenye kaunti 

Malulu amewarai wakaazi wa eneo bunge lake la Malava kumpa nafasi nyingine ya kuongoza eneo bunge hilo kwenye uchaguzi mkuu ujao ili kuendeleza ajenda alizo kuwa nazo ikiwemo swala la elimu

By Javan Sajida

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE