Kwa mara nyingine mjumbe wa Kiminini daktari Chris Wamalwa ametoa wito kwa rais  kuyaruhusu maeneo ya kuabudu kuendelea kufanya kazi,

Akizungumza mda  mchache  na wanahabari baada ya kuwasili nyumbani kwake ,dkt Wamalwa  amelisikitikia swala la waumini kusalia nyumbani siku za ibada  huku shughli zingine zikiiendelea huku akisema kuwa ni ibada pekee itakayoikomboa taifa kutokana na Janga la korona,

Mjumbe huyo aidha ametilia hofu kwamba huenda visa vya upotovu wa nidhamu haswaa miongoni mwa vijana vikapanda juu kutokana na wao kukosa kupata ushauri wa kidini,

Hivyo basi daktari Wamalwa  amemuomba rais Uhuru Kenyatta  kuubadili msimamo wake wa hapo awali wa kuyafunga maeneo ya kuwabudu kwa mda  na kuwaruhusu wauminui kuendelea na ibada kama  ada,

Usemi wa mjumbe huyo unakujia siku moja tu baada ya usemi sawia na huo kutoka kwa  askofu wa kanisa la ki Anglikana Philip  Mechumo.

By Hillary Karungani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE