Baadhi ya wazazi katika shule ya upili ya Wasichana ya Cardinal Otunga kwenye Kaunti ya Bungoma wameushtumu uongozi wa shule hiyo kwa kuwatimua wanafunzi watano wa kidato cha tatu kwa madai ya kutumia dawa za kulevya.

Baadhi yao waliozungumza na Kituo hiki kwa njia ya simu, wameikosoa Bodi ya shule hiyo kwa kuwalazimisha wanafunzi kukubali makosa ambayo hawakuhusika na kuwatimua hata bila kuwapa nafasi kujieleza jinsi anavyoeleza mzazi huyu.

Usemi wake umerejelewa na mzazi mwingine akisema ripoti ya daktari inaashiria kuwa mwanawe hajawahi tumia dawa za kulevya kinyume na makosa yanayomkabili.

Aidha wazazi hao wamedai kushurutishwa kulipa karo yote iliyosalia kabla ya kuruhusiwa kuondoka shuleni na wanao.

Kwa Jumla ni wanafunzi watano waliotimuliwa shuleni humo kwa madai ya kutumia dawa za kulevya na njama ya kupanga mgomo.

 Story by Hillary Karungani

sadmin

By sadmin

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE