Kama moja wapo ya kujipanga kukabiliana na msambao na mkurupuko wa magonjwa mbalimbali  sasa waziri wa afya kaunti ya Bungoma Antony Walela ameombwa kuzihami hospitali  na zahanati zote katika kaunti  ya Bungoma  na vitanda vya kutosha.

Akizungumza ofisini mwake askofu mkuu kanisa la ki anglikana Philip Mechumo ametiilia shaka utepetevu ulioko katika wizara ya afya huku akisema kuwa  ipo haja ya sekta hiyo muhimu kufanyia marekebisho  miundo misingi  na vifaa ili kuwafikia hata watu wengi zaidi.

Kuhusu malumbano ya mara kwa mara ya wanasiasa katika kaunti ya Bungoma askofu Mechumo amewataka vigogo wa kisiasa ukanda huu kuweka vichwa pamoja kama wana nia ya  kuunda serikali mwaka wa 2022.

Askofu Mechumo aidha ametumia fursa hiyo kuwarai wakristo kote nchini kuiombea nchi haswaa msimu huu dunia inapopitia changamoto za kiuchumi kufuatia changa kuu la korona. 

By Hillary Karungani

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE