Wizara ya ulinzi ya israel imetangaza leo kwamba nchi hiyo imefaulu kuzindua satelaiti mpya ya ujasusi,

Inayosema itaiwezesha idara ya uchunguzi ya jeshi lake kupata taarifa bora za ujasusi.

Israel imekuwa ikiimarisha uwezo wake wa kijasusi ili kuwachunguza maadui zake kama vile iran ambayo inautizama mpango wake wa nyuklia kama kitisho. Satelaiti hiyo kwa jina ofek 16, ilirushwa kuelekea anga za juu mapema leo, kutoka eneo la kati ya Israel kwa kutumia kombora lililotengenezwa ndani ya Israel, ambalo limekuwa likitumika kurusha satelaiti za awali nchini humo. Wizara ya ulinzi ya israel

Imeitaja ofek 16 kuwa na uwezo ulioimarishwa Zaidi wa uchunguzi wa kijeshi.

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE