Mwakilishi maalum katika bunge la kaunti ya Kakamega Lucy Chogo amewataka viongozi wa akina mama kushirikiana kuwasaidia wasichana kukabili changamoto ya ukosefu wa visodo ambayo inachangia mimba za mapema
Akiongea katika shule ya upili ya Shiveye wadi ya Idakho Mashariki eneo Bunge la Ikolomani alipowahamasisha wasichana kuhusu siku ya hedhi, bi Chogo amewataka viongozi wa akina mama kutumia raslimali wanazozipata kuwafaa wasichana
Aidha amewataka wasichana kutopotoshwa na wazingatie elimu yao kwa manufaa ya maisha yao ya kesho
By Richard Milimu