Mvutano  unaendelea  kushuhudiwa   baina  ya  viongozi   wa  kisiasa   kutoka  eneo  bunge  la  Mumias  Mashariki     wakionekana  kutofautiana   kutokana  mahali    hospitali  ya  level  4  inastahili kuwekwa   eneobunge  hilo  baadhi yao  wakipendekeza   hospitali  ya  Makunga   ipandishwe  kiwango  cha  kuwa  level  4  huku  wengine  wakipendekeza  iwekwe  mjini  Shianda.

Wakizungumza  katika  kijiji  cha  Ikoli , eneobunge  la  Mumias  Mashariki   kwenye    mazishi  ya  Rodgers  Makokha  nduguye  mwanasiasa  kutoka  maeneo  hayo  Steven  Makokha  wanasiasa  hao  wananyosheana  kidole  cha  lawama   kutokana   na  pendekezo  la  kujengwa  kwa  hospitali  ya  level  4  eneobunge hilo. 

Kwa  upande  wake    mwakilishi  wadi  wa    Malaha/Makunga/ Isongo    Lucas  Radioli  aliyekuwa  amehudhuria  mazishi  hayo  aliwataka  wanasiasa   kukoma  kuingiza  siasa  katika  swala  la  hospitali  akidokeza  tayari  mikakati  imeanza  ya  kuiunda  hospitali  ya  Makunga  kuwa  kiwango  cha  level  4  na  kuongezea  bado  hospitali  ya  Shianda   itapandishwa   kiwango  cha  level  4  kutokana  na  chuo  cha  matibabu  kilicho  maeneo  hayo 

Naibu  wa  chifu  wa  kata ndogo  ya  Makunga James  Rapando  amewataka  wazazi  kutafuta  namna  ya  kuwapeleka  watoto  shuleni  kwa  muhula  wa  kwanza  kando  na  kuwatafutia  taasisi , na  vyuo  mbalimbali  vya  ufundi kwa  wanao  waliokamilisha  mitihanio  yao  ya  darasa  la  nane  na  kidato  cha  nne  mtawalia.

Ni  mazishi  yaliohudhuriwa  na  viongozi  mbalimbali  akiwemo  mbunge  wa  Lurambi  Askofu  Titus  aliyedinda  kuongelea  siasa  huku  akiwataka  wananchi  kuzifwata  sheria  za  wizara  ya  afya  kama  njia  mojawapo  ya  kupigana  na  janga  la  covid  19.

By James Nadwa

Related Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WP Radio
WP Radio
OFFLINE LIVE