Wito umezidi kutolewa kwa viongozi wa kisiasa nchini kuondoa siasa kwenye safari ya kufufua kiwanda cha kusaga sukari cha Mumias
Ni kauli yake mwaniaji wa kiti cha ubunge eneo bunge la Navakholo kaunti ya Kakamega Samuel Wekesa Wekulo
Akizungumza na kituo hiki Wekesa ameelezea masikitikio yake baada ya baadhi ya wanasiasa kuingiza siasa kwenye swala hili ambalo linamfaidi mkulima wa kawaida licha ya kusema anaunga mkono uwazi kuwepo kwenye mwekezaji atakaye saidia kufufua kiwanda hicho
Hii ni baada ya mwekezaji DEVKI kujiondoa kwa madai ya kuibgiliwa kisiasa baada ya kuonyesha nia ya kufufua kiwanda hicho kwa kuwekeza kima cha shilingi bilioni 5
By Javan Sajida