Baadhi wafwasi wa ANC pamoja na wachuuzi sokoni Makunga wilayani Navakholo sasa wanasisitiza kuwa Chama cha ODM kimepoteza umaarufu haswa eneo la Magharibi mwa nchi
Kwenye mahojiano ya kipekee na kituo hiki wanachama hao wanahusisha kuondolewa kwa seneta Malala kwenye kiti cha naibu wa walio wachache kwenye bunge la seneti kama pigo kwa chama hicho eneo hilo
Wanachama hao wameutaka uongozi wa ODM kutochukulia siasa za Matungu kama njia ya kumwadhibu seneta Malala
Wakaazi hao wahoji kuwa vyama vya kisiasa haswa ODM vina mazoea ya kuwadhalilisha vijana
By James Nadwa