Wanabodaboda wa eneo la Butali kata ya Matioli kaunti ndogo ya Malava kaunti ya Kakamega wameshauriwa kuungana pamoja katika vikundi ili waweze kusaidiana na kupata pia misaada kutoka kwa wafadhili mbali mbali
Benson Ngaira ambaye ni mwenyekiti wa wanabodaboda wa Township Stage amewashauri wenzake huku akiwataka kutilia maanani ushirikiano na kusaidiana ili waweze kuendelea kwa pamoja
Benson vilevile amezungumzia mojawapo ya changamoto kuu zinazowakumba kama wateja wao kurudisha pesa wanazotumiwa kwa simu kama nauli na kuwasihi waendeshaji wa pikipiki kuwa makini na abiria wao na pia wakati wapo barabarani
By Mary Owano